SHEREHE LAFANYIKA JIJINI MANCHESTER KUMUAGA SIR ALEX FERGIE

SHEREHE LAFANYIKA JIJINI MANCHESTER KUMUAGA SIR ALEX FERGIE
Mabingwa wa ligi kuu soka nchini Uingereza, Manchester United leo hii wamepiga bonge la sherehe kushangilia ubingwa wao wa 20 pamoja na kumuaga rasmi kocha wao aliyewafundisha kwa miaka 27 na kutwaa makombe 49 katika michuano mbalimbali.
Viongozi, wachezaji na mashabiki wa United leo hii wamepita mitaa mbalimbali ya jijini Manchester kushangilia ubingwa wao na kumuaga Ferguson kwa heshima kubwa.
Kocha Kibabu leo hii kaagwa rasmi na kubwaga manyanga ya kuwanoa United na kazi yake kumrithisha kocha ambaye amemhusudu kwa muda mrefu, David Moyes ambaye kwa sasa ni kocha wa Everton.
Manager Sir Alex Ferguson 
 
Ferguson amesitaafu huku akiwa tayari amesharejesha ubingwa alionyang`anywa na watani zake wa jadi Manchester City msimu uliopita na kupeleka adhaa kubwa kwa kocha wa City, Roberto Mancini ambaye kibarua chake kinaweza kuinga mchanga wakati wowote baada ya kufanya vibaya msimu huu.
Feguson amekaa na timu kwa miaka 27, ni ngumu kujua kama Moyes ataweza kukaa muda kama wake akiwa na United ama la.
Watu wengi walidhani Mreno Jose Mourinho angebeba mikoba ya Fergie lakini imekuwa taofauti kabisa.

Sod off: A child holds a sign with a message for Wayne Rooney 

Finale: Manchester United fans gather in Albert Square to greet the bus
Ndani ya Albert Square

Comments